Solomonitv brog ni Brog ya kisasa itakayo kuhabarisha habari zote katika Dunia hii,Kwa matangazo zaidi husisite kuwasiliana nami maana Bei ni nafuu sana habari whatsapp No +255 624 499 969 Au +255 759 290 764




Wazimbabwe wajitayarisha kwa uchaguzi Jumatat


Katika treni yendayo taratibu usiku kutoka Johannesburg kwenda mpakani na Zimbabwe,mazungumzo ni iwapo uchaguzi kesho Jumatatu(30.07.2018)unaweza kuleta mshangao na kuiangusha serikali inayoongozwa na chama cha ZANU-PF.
Wasafiri  wa  kawaida  waliobeba  mahindi, mablanketi  na  sabuni za  kufulia walikaa pamoja  na  wapiga  kura  wakielekea  nyumbani kwa  ajili  ya  uchaguzi wa  kwanza  nchini  Zimbabwe  tangu kiongozi aliyeongoza  nchi  hiyo  kwa  mkono  wa  chuma Robert Mugabe kuondolewa  madarakani miezi  minane  iliyopita.
Mabehewa  sita  ya  treni  hiyo iliondoka  katika  kituo  kikuu  cha mjini  Johannesburg  cha  Central Park mapema  jioni  ya  Ijumaa katika  safari  ya  masaa 15, ya  kilometa 600 katika  majira  haya ya  baridi.
"Watu wa Zimbabwe  wanahitaji  maisha  mapya  ili  waweze kusahau juu  ya maisha  magumu  tuliyopitia  chini ya  yule  mzee Mugabe," amesema  abiria  mmoja  Emile Manyikunike, mwenye umri  wa  miaka  36, akivalia  koti  la  baridi  la  ngozi lenye  rangi nyeusi na  fulana ya  kijani  yenye  picha  ya  Bob Marley.
"Watu walikuwa  wanapigwa na  polisi kwa  kutokubaliana  na serikali, na hata  hatukuweza  kuwaamini majirani  zetu  kwasababu kila  mtu  wa  pili  alikuwa  ni mpelelezi  wa  ZANU-PF," aliliambia shirika  la  habari  la  AFP.
SolomoniTv
Share:

0 comments:

Post a Comment